MOMBASA, KENYA: MCHUNGAJI AMUUA KWA KISU MKEWE NA YEYE KUJIUA
-
Tukio hili la kusikitisha limetokea siku ya leo wakati Ibada ya Jumapili ikiendelea katika Kanisa la Ground For Gods Gospel (3G) Ministries lililopo Kaunti ya Kisauni
-
Imeelezwa kuwa, Mchungaji Elisha Misiko alimshambulia kwa kisu mkewe aliyekuwa amekaa naye jirani kisha na yeye kujiua kwa kisu hicho hicho
-
Habari za awali zinaeleza kuwa, chanzo cha ugomvi uliopelekea mauaji hayo ni mgogoro wa ndoa huku Mchungaji huyo akiacha ujumbe wenye kurasa 17 unaoelezea mgogoro wao
-
Hata hivyo Polisi katika Kaunti ya Kisauni wamekataa kueleza kilichoandikwa na Mchungaji huyo kwa maelezo kuwa uchunguzi bado unaendelea
Comments
Post a Comment